VIJAMBO
HABARISHA JAMII KWA KILE KINACHOTOKEA
Monday, July 8, 2013
Wednesday, May 29, 2013
WANAFUNZI WAKIPIGA KURA ZA SIRI ILI KUWAFICHUA WALIMU WANAOFANYA MAPENZI NA WANAFUNZI SHULENI
KATIKA hali isiyo ya kawaida, wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyasubi, iliyopo Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, wamepiga kura za siri ili kuwafichua walimu wenye tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi wao shuleni hapo.
Uamuzi wa kupigwa kura hizo ulifikiwa hivi karibuni kwenye Kikao cha Baraza la Shule la Watoto ambacho kiliitishwa kwa lengo la kujadili vurugu zilizokuwa zikijitokeza shuleni hapo na kusababisha baadhi ya walimu kupigwa.
Wednesday, May 15, 2013
MITANDAO YA KIJAMII KAMA FACEBOOK UATHIRI WATU KISAIKOLOJIA- SOMA HAPA"
Facebook,
mitandao mingine ya kijamii pamoja na huduma ya ‘blackberry mesenger’
maarufu kama BBM huathiri watu kisaikolojia, husababisha ndoa kuvunjika
pamoja na usaliti katika uhusiano, wanasayansi wamebaini.
Utafiti
huo uliofanywa mwaka 2012 na wanasayansi wa nchini Israel umebaini kuwa
kwa wastani, wanawake wanatumia dakika 81 katika mitandao ya kijamii kwa
siku ukilinganisha na wanaume ambao hutumia dakika 64, huku watu wasio
na elimu wakionekana kuathirika zaidi na mitandao hiyo.
Tuesday, May 14, 2013
Friday, May 10, 2013
MAAJABU: PICHA ZA MIZOGA YA MBUZI NANE WACHINJWA MAKABURINI USIKU WA MANANE MOROGORO
Katika hali isiyo ya kawaida tumepokea taarifa kutoka kwa wafanyakazi wa manispaa kitengo cha makaburi ya kolla wakidai kwamba usiku wa manane wa kuamkia juzii mbuzi nane wamechinjwa eneo la makaburi ya kola mkoani morogoro

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mnamo tarehe 03 Mei, 2013 Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Wiliam Lukuvi (Mb) ilitoa Kauli ya
Serikali Bungeni Kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Sababu za kushuka kwa ufaulu wa Mtihani wa Kidato cha
Nne Mwaka 2012.
Kauli ya Serikali ilielekeza kuwa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yafutwe na yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011 ili Wanafunzi hao wawe katika mazingira yanayofanana na ya wenzao wa miaka iliyopita kwa kuwa mfumo uliotumika mwaka 2012 katika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika mwaka 2011 na miaka
iliyotangulia.
MAJINA 9 YA WATUHUMIWA WALIOLIPUA BOMU KANISANI-- ARUSHA

Imeripotiwa kuwa jumla ya watu 12 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Arusha kwa kutuhumiwa kuhusika na mlipuko wa bomu lililorushwa katika eneo la Kanisa la Mt Joseph Mfanyakazi katika parokia teule ya Olasiti siku ya Jumapili, Mei 5, 2013 na kusababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi wengine zaidi ya 60.
Ripota wa WAPO FM radio alisema majina ya watuhumiwa hao yametajwa kuwa ni:-
- Victor Ambrose Calist (20, mkazi wa Kwa Mrombo, Arusha)
- Joseph Yusuph Lomayani (18, mkazi wa Kwa Mrombo, Arusha)
- George Bartholomeo Silayo (26, mkazi wa Olasiti, Arusha)
PICHA ZA MAZISHI YA WALIOKUFA KATIKA MLIPUKO WA BOM KATIKA KANISA LA MT JOSEPH ARUSHA.
Thursday, May 9, 2013
HUYU NDIYE GAIDI ALIYERUSHA BOMU KANISANI, AFUNGA NA KUNENA MANENO MAZITO....SOMA HAPA..!!

Kijana aliyemkimbiza hadi kumkamata mtu anayedaiwa kuhusika na kulipua bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, jijini Arusha akiwaelezea wananchi ilivyokuwa.
ALIYEMKIMBIZA hadi kumkamata mtu anayedaiwa kuhusika na kulipua bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, jijini Arusha Jumapili iliyopita na kuua watu 3 na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa ameibuka.
Kijana huyo ambaye wakati akizungumza na watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari jijini Arusha juzi alisahau kutaja jina lake, alisema kuwa shughuli ya kumnasa mtuhumiwa huyo haikuwa lelemama hata kidogo.WANAFUNZI WA UMBWE SEKONDARI WAGOMA KULA KWA MADAI YA KUTORIDHISHWA NA MKUU WAO SHULE...!!
MGOGORO umeibuka katika Shule ya Sekondari Umbwe kati ya wanafunzi wa kidato cha tano na uongozi wa shule hiyo hali iliyosababisha baadhi ya wanafunzi kugoma kula na kufanya maandamano wakishinikiza kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa lengo la kutatua kero zilizoko shuleni hapo.
Kutokana na mgogoro huo, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Dk. Ibrahim Msengi aliyefika shuleni hapo kuutatua, alimtaka Ofisa Elimu Mkoa Kilimanjaro kupeleka wakaguzi katika shule
Kutokana na mgogoro huo, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Dk. Ibrahim Msengi aliyefika shuleni hapo kuutatua, alimtaka Ofisa Elimu Mkoa Kilimanjaro kupeleka wakaguzi katika shule
VIOJA VYA WANAFUNZI "KAMA HAKUNA NIDHAMU MASHULENI, MATOKEO YATAENDELEA KUFUTWA KILA MWAKA.....!!"

Kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya wanataaluma na wanasiasa kuhusu suala la elimu hapa nchini.....
Wanataaluma wengi wanapinga uamuzi wa serikali kuyafuta matokeo ya kidato cha nne kwa madai kwamba hilo siyo suluhisho la la tatizo ......
HII NDIO HALI YA WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA WALIOJIUNGA NA JKT, ANGALIA MWONEKANO WA WAKIWA MAFUNZONI...!!

Hawa ni wanaume wakirushwa kichura na kamanda wa mafunzo, huko c mchezo......
VURUGU HUKO RUAHA WILAYA YA KILOSA
Taarifa nilizo zipata muda huu kutoka kwa mmoja wa wanakijiji cha Ruaha wilaya ya kilosa mkoani Morogoro zinaangaza kuwa kumetokea vurugu na mpaka muda huu mabomu yanarindima kila upande. Vurugu hizo zilizo sababisha kupigwa mabomu ni vurugu za kisiasa.
Sababu za vurugu.
• Tarehe 24/4/2013 ulikuwa ufanyike uchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, mgombea wa Chadema alienguliwa na Afisa mtendaji wa kata ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi.
Sababu za vurugu.
• Tarehe 24/4/2013 ulikuwa ufanyike uchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, mgombea wa Chadema alienguliwa na Afisa mtendaji wa kata ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi.
ALIYEKUWA MHASIBU MKUU WA JAMBO LEO AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited, marehemu Vick Mgoyo
****************************************
MHASIBU Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts (T) Limited inayochapisha gazeti la Jambo Leo, Staa Spoti, Dar Metro na jarida la Jambo Brand Tanzania, Vicky Mgoyo (49), amefariki dunia.
Tuesday, May 7, 2013
TCU WAKIFUNGIA CHUO CHA KAMPALA INTERNATIONAL UNIVERSITY ( KIU ) KWA KUTOKIDHI VIGEZO
CHUO CHA KIU-DCC KUSIMAMISHWA KUTOA MAFUNZO YA SHAHADA ZA UZAMILI NA UZAMIVU
Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam (KIU-DCC) kilichopo Gongo la Mboto, Dar-Es-Salaam ni Chuo kilichopewa idhibati na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU). Kufuatia kuendesha mafunzo ya shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) kinyume cha utaratibu na kutokua na wahadhiri wa kutosha wenye sifa stahili, Tume katika mkutano wake wa hivi karibuni ulikiamuru Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam ifuatayo;
1. KIU isimamishe mara moja mafunzo yote ya shahada za juu (Postgraduate) ikiwa ni pamoja na Shahada za Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) katika kampasi ya Dar-es-Salaam.
Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam (KIU-DCC) kilichopo Gongo la Mboto, Dar-Es-Salaam ni Chuo kilichopewa idhibati na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU). Kufuatia kuendesha mafunzo ya shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) kinyume cha utaratibu na kutokua na wahadhiri wa kutosha wenye sifa stahili, Tume katika mkutano wake wa hivi karibuni ulikiamuru Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam ifuatayo;
1. KIU isimamishe mara moja mafunzo yote ya shahada za juu (Postgraduate) ikiwa ni pamoja na Shahada za Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) katika kampasi ya Dar-es-Salaam.
JESHI LA TANZANIA LIMESHATUA CONGO.....WAASI WA M23 WAANZA KUHAHA KWA KUJIKOSHA KWA WANANCH

Kwa mujibu wa mwandishi aliye na waasi wa m23, Diana Katabarwa kwenye Blog yake anamnukuu kiongozi wa kisiasa wa M23 Mr. Bisimwa akiwambia wakazi wa North Kivu kuwa majeshi ya Tanzania na South Africa nimajeshi dhalimu yaliyo jaa rushwa na hayawezi kuibadili Congo....
WAZIRI MKUU ATEMBELEA KANISA LA OLASITI ARUSHA NA KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA KANISA PAMOJA NA WAUMINI.
HATIMAYE BALOZI WA PAPA AONDOKA ARUSHA.

Mwakilishi wa Papa akiwa na Askofu Lebulu akitoka kwenye VIP ya Arusha Airport kuelekea kwenye ndege ya Precision .Ilikuwa ni dakika za majonzi na masikitiko kwa kundi lote lililokuwa limemsindikiza uwanja wa ndege Balozi wa Papa ambaye ameondoka leo mjini Arusha kuelekea Dar, baada ya kunusurika katika shambulio la bomu lililorushwa wakati akiwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi huko Olasiti Arusha.
NAY WA MITEGO AFANANISHWA NA DEM....CHID BENZ AMTUNGIA JINA NA KUMUITA " NEEMA WA MITEGO"

Ugomvi wa chini chini kati ya Chid benz na Ney wa mitego sasa umefikia pabaya....
Juzi Ney wa mitego alionja kichapo toka kwa mashabiki katika show yake mbagala....Inadaiwa kwamba Varangati hilo lilitokana na madai yake kwamba Chid benz ni shoga na ametoboa pua kama dem....
Mapema mchana huu Chidi Benz amefunguka kupitia ukurasa wake ya Facebook na kumtaka NEEMA WA MITEGO(Neema ni jina la kike ) aache kumtukana wala kumwandika message zozote.....Vinginevyo ataendelea kuambulia kichapo
Subscribe to:
Comments (Atom)
