Sunday, April 28, 2013

PIGO KWA TAIFA LA KENYA: MUTULA KILONZO AFARIKI DUNIA.

 
PICHA YA MAREHEMU MUTULA KILONZO
Mutula Kilonzo ambaye ni Senator wa Makueni amekutwa amefariki nyumbani kwake ambapo pia ni ranch anapofuga wanyama mbalimbali. wakiwemo SIMBA..
The late Mutula Kilonzo feeds his lions on fresh meat from his herd of livestock. His workers found him dead after they broke into the house when they discovered he was not waking-up from sleep.  PHOTOS | Stephen Mudiari
Kiongozi huyu wa Makueni alifika nyumbani kwake siku ya Ijumaa mida ya saa kumi jioni akiwa anaendesha gari lake yeye mwenyewe. Na baada ya kufika alisalimiana na wafanya kazi wake na baada ya hapo kama ilivyo kawaida yake alitembelea ranch yake na kuona wanyama wake wakiwemo simba aliokua anawafuga katika Ranch yake. Wakati huo wafanyakazi wake walikuwa wakimuandalia chakula (Msosi) ambapo ilipofika mida ya saa moja usiku alipewa chakula na kula na baadae kwenda kulala katika chumba chake.
Ilipofika siku ya Jumamosi asubuhi wafanyakazi waliamka na kumuandalia chakula au Breakfast kama kawaida na kutenga tayari wakisubiri Boss wao Mutula Kilonzo aamke, lakini muda ulionekana unenda saa nne!!!......saa tano!!! na Boss huyo alikuwa haja aamka. Ndipo wafanyakazi wake wakaamua kwennda kumwamsha na dhani ni baada ya kuona sio kawaida yake kulala hadi mida hiyo.
Walifika katika chumba alicholuwa amelala na kugonga bila mafanikio ........baadae waliamua kuvunja mlango na kumkuta Mutula Kilonzo akiwa amelala na Povu likiwa linamtoka mdomoni. Na ndipo walipochukua hatua za kutoa taarifa panapo husika ili kuweza kupata msaada.
 Na baada ya uchunguzi ikaonekana kuwa alikuwa ameshaaga Dunia muda mrefu.
Mutula Kilonzo hatuko nae tena
 Pigo kwa FAMILIA YAKE
Pigo kwa TAIFA LA KENYA
Pigo kwa DUNIA NZIMA
KUTOKANA NA MCHANGO WAKE
Photo: Raila and Kalonzo visit Mutula's home following his death
photo Mike Kariuki
Photo: Johnstone Muthama and Dalmas Otieno at Mutula home
photo Mike KariukiPhoto: Close friends and family members in sombre mood at Mutula home  
photo Mike KariukiPhoto: Police Officers maintain security inside cordon at Mutula house
photo Mike Kariuki
hapo juu ni picha mbalimbali za waombolezaji wakiwemo viongozi wastaafu wa serikali ya Kenya.
Raila Odinga anaonekana akiwa katika huzuni kubwa sana pamoja na mwenzake Kalonzo Musyola.

No comments:

Post a Comment